Sera za kila chama
-
Azimio La Umoja One Kenya Coalition
Vipaumbele
- Kufikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
- Elimu Bure kwa wote.
- Huduma ya afya bora kwa wote.
Uchumi
- Kukuza sekta ya kilimo, mifugo, uvuvi na uchumi wa bluu hadi asilimia 30 ya Pato la Taifa.
- Kuza bidhaa za "Zilizotengezwa Kenya" kwa kusaidia ukuaji wa biashara ndogo ndogo na za kati.
- Mpango wa "Kaunti Moja, Bidhaa Moja" kutegemea utengenezaji kama injini ya uundaji wa utajiri na ajira.
Ufisadi
- Kuboresha kwa haraka mamlaka ya kisheria na kiutawala.
- Kuongeza kasi ya kurejesha mapato ya rushwa na uwepo wa fedha haramu.
- Kutovumilia rushwa.
Madeni
- Kupunguza kasi ya ulimbikizaji wa madeni.
- Boresha sera za usimamizi wa madeni.
- Kuendeleza mazungumzo ya msamaha wa madeni.
Ajira
- Kutumia vizuri idadi kubwa ya vijana kwa ustawi
- Kuboresha tija katika sekta ya viwanda na kusaidia uzalishaji wa ajira katika sekta hiyo.
- Wekeza katika teknolojia zinazoibukia ambazo zitatoa fursa za ajira kwa vijana wa Kenya.
Kawi
- Punguza gharama ya umeme.
- Tathmini ushuru na kodi za bidhaa za petroli.
- Kuongeze utafutaji wa mafuta na gesi kwenye nchi kavu na baharini.
Afya
- Huduma ya afya bora kwa wote.
- Kukuza uzalishaji wa ndani wa dawa na pembejeo nyingine zinazohusiana na afya.
- Kuboresha mazingira ya kazi na malipo ya wataalamu wa afya.
Uhalifu na usalama
- Kuhakikisha utekelezaji madhubuti wa mageuzi ya polisi.
- Kuwafunza angalau maafisa sita wa polisi katika kila kituo cha polisi kushughulikia uhusiano wa polisi na vijana.
- Boresha sheria na sera kuhusu usalama na usalama mtandaoni.
Elimu
- Kutoa elimu bure kuanzia chekechea hadi chuo kikuu.
- Toa mlo mmoja kwa siku kwa watoto wa chekechea na madarasa ya mwanzo ya shule za msingi
- Kukuza uhusiano wa kufanya kazi kati ya taasisi za elimu na utafiti na viwanda.
Usambazaji wa maji
- Wekeza na kukuza uvunaji wa maji ya mvua na udhibiti wa mafuriko.
- Kupanua miundombinu ya mabwawa na umwagiliaji.
- Kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama kwa kila shule na boma
Gharama ya maisha
- Tathmini gharama ya mafuta, unga na nishati katika siku 100.
- Kuongeza uwezo wa kusambaza umeme na kupunguza upotevu wa gridi kutoka asilimia 23 hadi 10.
- Weka mazingira wezeshi ya kupata chakula, mavazi, malazi na mahitaji mengine ya kimsingi kwa bei nafuu.
-
Roots Party of Kenya
Vipaumbele
- Kuendesha serikali yenye faida kupitia kuhalalisha na kudhibiti utumiaji wa bangi kiviwanda
- Kuunda majimbo 8 ambayo yatasimamiwa na serikali zao za shirikisho.
- Sitisha katiba, ili kuwapa Wakenya fursa ya kuchagua sheria inayowafaa.
Uchumi
- Uchumi wa saa 24 wa zamu ya saa nane, siku nne kwa wiki.
- Kuongeza bajeti ya serikali kupitia mapato ya fedha za kigeni kutokana na mauzo ya katani ya viwandani.
- Pata mapato kupitia ufugaji wa nyoka na kuuza nje nyama ya mbwa.
Ufisadi
- Kuanzisha hukumu ya kifo inayotumika kwa watu wanaopatikana na hatia ya rushwa.
- Kutovumilia rushwa.
Madeni
- Lipa deni la Kenya haraka kwa mapato kutoka kwa kuhalalisha na usafirishaji wa bangi ya viwandani.
- Mkopo huo utalipwa kwa awamu 30 kati ya Januari 2021 hadi Julai 2035.
- Epuka madeni kwa kutumia mapato yaliyopatikana kutokana na kuhalalisha bangi ili kuongeza mapato ya serikali.
Ajira
- Unda fursa za Uwekezaji na ajira kwa kuhalalisha bangi
Kawi
- Tumia katani ya Viwanda kuzalisha nishati ya kibayolojia.
- Kupunguza gharama ya nishati kwa kupunguza kodi na kushughulikia mzigo wa madeni.
Afya
- Huduma za afya na lishe ya bure kwa wazee, walio katika mazingira magumu na wajawazito.
- Boresha matibabu na udhibiti wa Alzheimer's, saratani, ugonjwa wa kupooza kwa ubongo na kifafa kwa kutumia moja ya bidhaa za katani za viwandani.
- Kutanguliza utafiti na maendeleo katika kampuni za dawa zinazomilikiwa na Kenya.
Uhalifu na usalama
- Kuwalipa polisi vizuri ili kupunguza rushwa.
Elimu
- Wape wazazi chaguo la masomo ya nyumbani na kurahisisha mchakato wa usajili.
- Boresha mfumo wa elimu wa CBC nchini Kenya.
Usambazaji wa maji
- Kuboresha miundombinu ya majisafi na majitaka.
Gharama ya maisha
- Tengeneza fursa za ajira na uwekezaji.
- Punguza kodi na gharama ya nishati.
-
Chama cha Agano
Vipaumbele
- Unda taasisi zitakazomaliza ubadhirifu wa fedha na kukomesha ufisadi.
- Hakikisha kwamba haki za wasio na sauti na waliotengwa zinazingatiwa.
- Punguzo la ushuru kwa Wakenya kusaidia kudhibiti gharama ya maisha.
Uchumi
- Kupeleka bajeti kwa halmashauri za vijiji badala ya Hazina na Ikulu.
- Weka mazingira mazuri kwa sekta binafsi na watu binafsi kuanzisha biashara.
Ufisadi
- Fanya ripoti za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu kuwa ushahidi wa msingi wa matumizi mabaya ya ofisi na msingi wa kuwashtaki watumishi wa umma walio wafisadi
- Kesi zote za ufisadi zitashughulikiwa ndani ya miezi mitatu.
- Tume ya Maadili na Kupambana na Rushwa kupewa mamlaka ya kuendesha mashtaka.
Madeni
- Majadiliano kwa lengo la kupanga upya ulipaji wa deni na wakopeshaji.
- Tumia fedha zilizopatikana kutokana na shughuli za kifisadi kulipa madeni ya nje.
- Kurejesha fedha zilizofichwa nje ya nchi ili kusaidia kulipa deni la nje .
Ajira
- Tekeleza sheria ya maudhui ya humu nchini kwa kuongeza kiwango cha juu cha kandarasi zinazotolewa kwa makampuni ya kigeni hadi zaidi ya $8.5 milioni (Ksh1 bilioni).
- Punguzo la kodi kwa makampuni yanayoajiri wanawake na vijana.
- Kuharakisha utekelezaji wa mpango wa Kanda Maalum ya Kiuchumi ili kuhimiza wageni,makampuni ya kuanzisha viwanda vya utengenezaji nchini Kenya.
Kawi
- Kusaidia matumizi ya nishati ya jua nje ya gridi ya taifa.
- Kufanya nishati kuwa bei nafuu kwa kushughulikia rushwa katika sekta ya nishati.
Afya
- Unda tume ya kitaifa ya afya ili kudhibiti kupanda kwa gharama za afya.
- Kutoa ruzuku kwa michango ya Mfuko wa Kitaifa wa Bima ya Afya kwa kila familia Kenya.
Uhalifu na usalama
- Kuboresha maisha na mazingira ya kazi ya polisi.
- Fanya vikosi vya usalama kuwa vya kisasa ili kuendana na uhalifu wa kisasa.
- Punguza msongamano wa magereza na kuboresha hali ya maisha na kazi ya maafisa wa magereza
Elimu
- Kuanzisha kipengele cha maadili katika mtaala.
- Elimu ya bure katika ngazi zote.
- Walimu wawezeshwe kidijitali kufanya kozi za kujiongeza masomo
Usambazaji wa maji
- Maeneo kame kupokea maji ya bomba kwa ajili ya umwagiliaji.
- Kuondoa tozo dhidi ya vifaa vyote vya kuvuna maji ya mvua.
- Kukuza upandaji miti upya.
Gharama ya maisha
- Msamaha wa jumla wa 50% kwa PAYE kwa Wakenya wote.
-
Kenya Kwanza Alliance
Vipaumbele
- Tenga $427 milioni (Ksh50 bilioni) kila mwaka ili kutoa mikopo kwa biashara ndogo ndogo na za kadri kwa njia rahisi na inayotegemeka
- Kurekebisha Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ili kubadilisha mchango kwa familia/nyumba badala ya watu binafsi.
- Mtandao wa bure ndani ya miaka mitano.
Uchumi
- Komesha ushuru unaorudiwa
- Fanya leseni ya biashara na eneo kuwa haki.
- Weka sera thabiti ya ulinzi wa huduma za kifedha ili kuwalinda Wakenya dhidi ya wakopeshaji walaghai.
Ufisadi
- Kuzipa uhuru taasisi zinazohusika na vita dhidi ya rushwa.
- Taarifa za wafanyabiashara wanaofanya biashara na serikali kuwekwa wazi.
- Shirikiana na nchi nyingine kusaidia kurejesha mali zilizoibiwa.
Madeni
- Kuimarisha uwezo wa serikali wa kukopesheka kutoka nje na kuongeza upatikanaji wa mikopo nafuu, na kuacha vyanzo vya mikopo vya ndani kwa sekta binafsi.
Ajira
- Wekeza kwenye kilimo ili kutengeneza ajira zaidi.
- Anzisha Kituo cha Maendeleo ya Biashara cha MSME katika kila kata na bustani ya viwanda.
- Kuanzisha kituo cha ukuzi wa biashara katika kila taasisi ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi.
Kawi
- Weka mfumo wa kisheria wa kulinda hazina ya uimarishaji wa mafuta.
- Unda vivutio vya kupitishwa kwa mifumo ya usafiri wa umma ya umeme katika miji na miji yote.
- Kuharakisha maendeleo ya rasilimali ya kawi ya mvuke
Afya
- Huduma ya afya ya msingi inayofadhiliwa kikamilifu.
- Kuanzisha mfuko wa kitaifa wa magonjwa sugu.
- Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya wa lazima.
Uhalifu na usalama
- Imarisha uangalizi wa polisi na kuteua mchunguzi atakayezingatia ukiukwaji wa haki za binadamu kwa vijana.
- Bima ya maisha kwa maafisa wa polisi iwapo watafariki wakiwa kazini.
- Mfuko wa hisani wa kuchangia familia za maafisa walioaga dunia na wagonjwa mahututi.
Elimu
- Lipia mafunzo ya ualimu kazini.
- Tathmini mfumo wa sasa wa maendeleo ya kitaaluma kulingana na mitihani.
- Kupunguza pengo la sasa la upungufu wa walimu 116,000 ndani ya miaka miwili ya kifedha.
Usambazaji wa maji
- Maji yatapewa kipaumbele kwa ruzuku ya mradi/ufadhili wa masharti nafuu.
- Hamisha mwelekeo kutoka kwa mabwawa makubwa hadi kwenye miradi ya maji ya kijamii huku msisitizo ukiwa katika kuvuna na kurejeleza
Gharama ya maisha
- Kuongeza tija ya kilimo ili kupunguza gharama ya maisha.








