Moja kwa moja, Marekani yaishambulia Iran kwa usiku wa saba mfululizo

Jeshi la Marekani limesema linazidisha mashambulizi ili kudhoofisha vikosi vya kijeshi vya Iran, huku Iran ikiripoti milipuko karibu na Mlango Bahari wa Hormuz.

Muhtasari

Ruka Video uendelee
  • xx
  • xx
  • xx
  • Lungu
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • xx
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Asha Juma

  1. Kombe la Dunia: Marekani yatetea bango la wachezaji wa Argentina

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Ikulu ya Marekani imetetea timu ya taifa ya Argentina baada ya wachezaji wake kuonyesha bango lililoandikwa "Las Malvinas son Argentinas" ("Visiwa vya Falklands ni vya Argentina") kufuatia ushindi wao dhidi ya England katika nusu fainali ya Kombe la Dunia.

    Hatua hiyo imekosolewa na Uingereza huku Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) likitatarajiwa kuchukua hatua za kinidhamu.

    Andrew Giuliani, mkuu wa kikosi kazi cha FIFA cha Ikulu ya Marekani, amesema wachezaji hao walikuwa wakitumia haki yao ya uhuru wa kujieleza chini ya Marekebisho ya Kwanza ya Katiba ya Marekani walipokuwa nchini humo, kwa mujibu wa BBC.

    Bango hilo linarejelea madai ya muda mrefu ya Argentina kuhusu visiwa vilivyoko kusini mwa Bahari ya Atlantiki, vinavyojulikana kwa Kiingereza kama Falkland Islands na kwa Kihispania kama Las Malvinas.

    Serikali ya Uingereza imekosoa kitendo hicho, huku Ikulu ikisisitiza kwamba Visiwa vya Falklands "kwa hakika ni" vya Uingereza na kuunga mkono wito wa FIFA kuchunguza iwapo bango hilo lilikiuka kanuni za shirikisho hilo zinazokataza kauli za kisiasa wakati wa mechi.

    Serikali ya Visiwa vya Falklands pia imeeleza kusikitishwa kwake na kuitaka FIFA kuichukulia hatua timu ya Argentina, ikisema haitaki kutumiwa kama "mpira wa kisiasa".

    Soma Zaidi:

  2. Tumelenga kituo cha Marekani na madaraja kadhaa nchini Bahrain - Iran

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Jeshi la Iran limetangaza kwamba katika awamu ya kumi na tano ya Operesheni "Shine", limelenga "maeneo ya ndege pamoja na matangi ya mafuta, katika kituo cha Sheikh Issa nchini Bahrain" kwa kutumia ndege zisizo na rubani za kujilipua.

    Taarifa hiyo pia ilidai kwamba madaraja kadhaa nchini Bahrain yalilengwa na mashambulizi ya ndege zisizo na rubani. Hata hivyo, si maafisa wa Bahrain wala Marekani hakuna ambaye ametoa maoni juu ya kiwango cha uharibifu au uwezekano wa kuwepo kwa majeruhi.

    Soma Zaidi:

  3. Mwanaharakati wa India aliyegoma kula kwa siku 20 apelekwa hospitalini kwa nguvu

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Mwanaharakati na msomi wa India Sonam Wangchuk, ambaye alikuwa kwenye mgomo wa kula kwa siku 20 zilizopita huko Delhi, ameondolewa kwa nguvu kutoka eneo lake la maandamano.

    Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 59 alikuwa akiandamana kuunga mkono harakati za kejeli mtandaoni zinazoitwa Cockroach Janta Party (CJP) zinazotaka mageuzi ya kielimu. Waandamanaji walikuwa wamepanga maandamano hadi bunge la India siku ya Jumatatu.

    Wangchuk alikuwa amegoma kula chakula wakati wa kiangazi chenye joto kali, huku akila chumvi na maji tu. Alikuwa amepunguza uzito zaidi ya kilo 9 na alikuwa na maumivu makali.

    Mwanzilishi wa CJP Abhijeet Dipke sasa ameanza mfungo usiojulikana badala yake. Anasema maandamano ya kuelekea bungeni yataendelea na amemtaka Waziri Mkuu Narendra Modi ajiuzulu.

    Dipke aliambia BBC kwamba alikuwa ameenda nyumbani kwa rafiki yake asubuhi ili kupumzika wakati polisi walipofika na kukataa kumruhusu aondoke.

    Video kutoka kwenye tovuti ya maandamano siku ya Jumamosi zilionyesha machafuko yakizuka kabla tu ya saa 1:30 kwa saa za huko (02:00 GMT) wakati polisi kadhaa na wanajeshi walipoingia ghafla kwenye jukwaa ambalo mwanaharakati huyo alikuwa amelala. Waandamanaji waliojaribu kuwazuia walisukumwa mbali.

    Walimfunika kwa mapazia ya shuka kabla ya kumtoa jukwaani. Dakika chache baadaye, ambulensi ilionekana ikiondoka kwa kasi.

    Mke wa mwanaharakati huyo Gitanjali Angmo baadaye alichapisha kwenye mtandao wa X kwamba alikuwa "katika hospitali ya Safdarjung ambapo amelazwa".

    Soma Zaidi:

  4. Marekani yaishambulia Iran kwa usiku wa saba mfululizo

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Jeshi la Marekani limesema limefanya mashambulizi kwa usiku wa saba mfululizo dhidi ya Iran tangu Rais Donald Trump atangaze makubaliano ya kusitisha mapigano kwa muda "yamefutiliwa mbali".

    Katika taarifa iliyowekwa kwenye mtandao wa X, Kamandi Kuu ya Marekani (Centcom) iliandika kwamba vikosi vyake "vimeshambulia maeneo ya uchunguzi, miundombinu ya vifaa vya kijeshi, maghala ya silaha yaliyopo chini ya ardhi, na uwezo wa kijeshi wa majini".

    Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) lilisema meli mbili za mafuta zililipuka katika Mlango-Bahari wa Hormuz wakati zikipita kwenye sehemu ya njia ya meli iliyokuwa na mabomu ya ardhini. Taarifa hiyo ilipuuzwa na Hata hivyo, Centcom ilisema kuwa taarifa hiyo si ya kweli.

    Vikosi vya kijeshi vya Jordan vilisema vilidungua makombora 10 ya Iran yaliyorushwa kwenye anga yake usiku huo, ingawa hakukuwa na majeruhi wala uharibifu wowote.

    Centcom ilisema kuwa ilimaliza mashambulizi yake saa 21:30 kwa saa za Marekani Mashariki (02:30 BST) baada ya kufanya mashambulizi hayo kwa muda wa saa kadhaa.

    Katika taarifa yake, Centcom ilisema: "Vikosi vya Marekani vilitumia ndege za kivita, ndege zisizo na rubani, na meli za kivita pamoja na vifaa vingine katika operesheni hiyo."

    Shirika la habari la serikali ya Iran, Fars, lilisema meli mbili za mafuta "zililipuka na kushika moto wakati zikipita kwenye njia iliyokuwa na mabomu ya ardhini kusini mwa Mlango wa Hormuz". Baadaye, Centcom iliandika kwenye X: "Kama madai mengi ya IRGC, hii si kweli."

    Usafirishaji wa meli katika Mlango muhimu wa Hormuz umesitishwa kwa kiasi kikubwa kutokana na kuendelea kwa mashambulizi ya kulipizana kisasi kati ya vikosi vya Marekani na Iran.

    Soma Zaidi:

  5. Hujambo. Karibu katika matangazo yetu mubashara tarehe ni 18/07/2026.