Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Moja kwa moja, Marekani yashambulia kwa siku 11 mfululizo; mifumo ya ulinzi wa anga yawashwa katika maeneo kadhaa ya Iran

Mbali na miji ya pwani ya kusini mwa Iran ambayo imekuwa ikishuhudia mashambulizi ya Marekani kwa wiki kadhaa, ulinzi wa anga pia uliripotiwa kuanzishwa Tehran Jumatano asubuhi.

Moja kwa moja

Lizzy Masinga

  1. Rais wa Ukraine amtimua Mkuu wa Jeshi, Oleksandr Syrskyi

    Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, amemwondoa Mkuu wa Majeshi ya Ukraine, Oleksandr Syrskyi, kutoka wadhifa wake.

    Hatua hiyo imekuja siku chache tu baada ya kuondolewa kwa Waziri wa Ulinzi aliyekuwa maarufu, Mykhailo Fedorov, hatua iliyosababisha maandamano katika maeneo mbalimbali nchini humo.

    Awali kulikuwa na uvumi kwamba kuondolewa kwa Fedorov kulihusiana na mgogoro kati yake na Syrskyi, na baadaye taarifa hizo zikathibitishwa.

    Fedorov, mwenye umri wa miaka 35, amekuwa akisifiwa kwa kuleta mageuzi makubwa katika Wizara ya Ulinzi, kuimarisha uwezo wa jeshi la Ukraine na kuongoza juhudi za kupambana na rushwa.

    Kwa upande mwingine, Syrskyi, mwenye umri wa miaka 60, anaonekana na wengi nchini Ukraine kama kamanda mwenye mtazamo wa kijeshi wa enzi za Umoja wa Kisovieti, ambaye hakuwa tayari kutekeleza mabadiliko makubwa ndani ya jeshi.

    Nafasi yake imechukuliwa na Jenerali Mykhailo Drapatyi, mwenye umri wa miaka 43, ambaye anajulikana kwa uzoefu wake mkubwa vitani na umaarufu miongoni mwa wanajeshi.

    "Nitafanya kazi kwa uwajibikaji, kwa umakini wa hali ya juu, na kwa heshima kwa wale wote wanaolinda nchi yetu leo," Drapatyi aliandika kwenye ukurasa wake wa Facebook.

    Pia alimshukuru Syrskyi "kwa kazi yake ya muda mrefu ya kuimarisha jeshi la Ukraine," akiongeza kuwa, "Nilikulia ndani ya jeshi hilo."

    Katika ujumbe wa video aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii usiku wa Jumanne, Rais Zelensky alimshukuru Syrskyi kwa mchango wake katika kampeni za kijeshi, ikiwemo nafasi yake muhimu katika kutetea kwa mafanikio mji mkuu wa Kyiv wakati wa siku za mwanzo za uvamizi kamili wa Urusi mwaka 2022.

    Unaweza kusoma;

  2. Vita vya Iran vimeigharimu Marekani dola bilioni 37.5 kufikia sasa - Waziri wa ulinzi

    Vita na Iran vimeigharimu Marekani takriban dola bilioni 37.5 (pauni bilioni 28) hadi sasa – ambalo ni ongezeko la karibu dola bilioni 8 tangu makadirio ya mwisho mwezi Mei, Waziri wa Ulinzi Pete Hegseth amesema.

    Hegseth aliiambia Kamati ya Matumizi ya Seneti kwamba ilikuwa muhimu kwa wabunge kuidhinisha ufadhili mwingine wa dola bilioni 87 katika bunge la Pentagon, huku dola bilioni 67 kati ya hizo zikielekezwa kwa shughuli za Mashariki ya Kati.

    Kikao hicho kilivurugwa mara kadhaa na waandamanaji wa kupinga vita na kumalizika kwa mapigano kati ya waziri wa ulinzi na seneta. Ilikuwa mara ya kwanza kwa Hegseth kuonekana Capitol Hill tangu uadui kati ya Marekani na Iran uanze tena wiki iliyopita na unakuja baada ya wanajeshi watatu wa Marekani kuthibitishwa kuuawa katika eneo hilo.

    Ikulu ya White House iliiomba Bunge mwezi Aprili dola trilioni 1.5 kwa Pentagon katika mwaka ujao wa fedha, ambayo ingeongeza matumizi ya kijeshi ya Marekani hadi kiwango cha juu zaidi katika enzi ya kisasa.

  3. Marekani yatangaza kumalizika kwa awamu ya 11 ya mashambulizi yake

    Saa moja baada ya kutangaza kuanza kwa mashambulizi yake dhidi ya Iran, Kamandi Kuu ya Marekani (CENTCOM) ilitangaza kukamilika kwa awamu ya kumi na moja ya mashambulizi hayo.

    Siku ya Jumatano asubuhi, wakati mashambulizi hayo yakianza, kulikuwa na ripoti za milipuko kadhaa katika miji kadhaa ya kusini mwa Iran.

    Kwa mara ya kwanza katika kipindi cha usiku wa kumi na moja , Tehran pia ilishuhudia kuwashwa kwa mifumo ya ulinzi wa anga siku ya Jumatano asubuhi, lakini hakuna maelezo yoyote yaliyotolewa hadi sasa kuhusu shambulio lolote linaloweza kuwa limeilenga mji mkuu huo wa Iran.

    Miji mingine ambayo iliripotiwa kushambuliwa ni pamoja na Sirik, Chabahar, Bushehr, Mahshahr, Konarak, Tabriz, Behbahan, na Omidieh.

  4. Natumai hujambo na karibu katika taarifa zetu za moja kwa moja